Sera ya Mitaala Mipya ya Elimu ikipitishwa inatarajiwa kuanza kutekelezwa Januari 2024 kama mapendekezo yaliyopo hayatabadilishwa ambapo miongoni mwa mapendekezo hayo ni ya mkondo wa mafunzo ya amali ambayo yatamsaidia mhitimu kujiajiri na kuajiriwa.
Kauli hiyo imetolewa leo Oct 10 mwaka 2023 jijini Dodoma na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Adolfu Mkeda katika Mkutano wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Wamiliki wa Shule Zisizo za Serikali wenye lengo la kusikiliza, kufahamu na kutatua changamoto zilizomo kwa kushirikiana na kutoka na Azimio moja.
Profesa Mkenda amewataka wamiliki hao wa shule binafsi kuwekeza katika Mkondo wa shule za Mafunzo ya Amali kwani mafunzo hayo yanahitaji uwezeshaji toshelevu na kama kuna sehemu watahitaji serikali iwasaidie watoe maoni yao na serikali ipo tayari kuwasikiliza.