MAHOJIANO MAALUM NA ROSTAM AZIZ LEO SAA TATU USIKU - AZAM TV

 


Mfanyabiashara na mwanasiasa maarufu kutoka Tanzania, Rostam Aziz, anatarajiwa kuzungumza leo kupitia Azam TV  (UTV) katika kipindi maalum cha mahojiano.


Kwa mujibu wa tangazo rasmi, mahojiano hayo yatafanyika leo Ijumaa, tarehe 5, Septemba 2025 kuanzia saa 3:00 usiku kupitia Runinga ya Azam.

Ingawa hakujatolewa dondoo rasmi za mada zitakazojadiliwa, mahojiano haya yanakuja katika kipindi ambacho hivi karibuni aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, amekuwa akimshambulia Rostam hadharani akimhusisha na tuhuma mbalimbali.

Watazamaji wanatarajiwa kufuatilia kwa karibu kusikia maoni na ufafanuzi wa Rostam kuhusu masuala ya kibiashara, kisiasa na mada moto zinazomhusu.

👉 Usikose kutazama Azam TV leo saa 3:00 usiku.
Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA