Na Bora Mustafa,Arusha.
Mkuu
wa Mkoa wa Arusha, CPA Amos Makalla, ametoa wito kwa madiwani wa Jiji
la Arusha kushikamana, kushirikiana na kuweka kando tofauti za kisiasa
ili kuwatumikia wananchi kwa ufanisi. Amesema uchaguzi sasa umekwisha na
kilichobaki ni kazi ya kuwahudumia wananchi waliowachagua.
Aidha,
RC Makalla amesisitiza umuhimu wa kusimamia miradi yote ya maendeleo
iliyopo chini ya Jiji pamoja na ile ya kata. Ametoa mfano wa miradi
aliyoitembelea, ikiwemo jengo la soko la Kilombero, na ameelekeza kuwa
miradi hiyo ikamilike kwa wakati kama ilivyopangwa. Ametaka baraza la
madiwani lihusishwe moja kwa moja katika usimamizi wake.
Amesema
pia kuwa ujenzi wa jengo la Jiji la Arusha unatarajiwa kukamilika
kufikia Mei 2026, na hivyo akawasihi Meya pamoja na madiwani kuhakikisha
wanashirikiana katika kukamilisha kazi hiyo kwa viwango vinavyostahili.
Pamoja
na hayo, RC Makalla amesema haiwezekani kuwa na uwanja mzuri wa mpira
katika mkoa wa Arusha halafu mkoa huo ukose timu ya kushiriki mashindano
makubwa. Ametoa wito wa kuwa na timu imara itakayowakilisha vyema mkoa
huo.
Hata
hivyo, amewataka madiwani kushuka kwa wananchi, kuwasikiliza kero zao
na kuwashukuru kwa kuwatupa kura za kuwachagua. Amesema wananchi
wanamwona diwani kama kiongozi wao, mshauri wao, na mlezi wa maendeleo
katika maeneo yao.
Aidha,
RC Makalla amesisitiza kuwa madiwani wanapaswa kuzingatia kwa makini
maombi ya wananchi, masuala ya mikopo ya vikundi, miundombinu ya
barabara pamoja na changamoto zingine zinazowakabili. Ametoa wito kwa
Jiji kushirikiana kwa karibu na TARURA katika kutatua changamoto hizo.
Kwa
upande mwingine, Makalla amesema suala la usafi halipaswi kuchukuliwa
kwa uzito mdogo. Amesisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuandaa utaratibu
madhubuti wa kuhakikisha Jiji la Arusha linakuwa safi wakati wote, kwa
kuwa ni Jiji la kimkakati linalotegemewa kwenye sekta ya utalii.






Post a Comment