NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI DKT. CHAYA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI WA GATSBY


Na, Mwandishi wetu.

 

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji (OR-MU), Mhe. Dkt. Pius Chaya, amefanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Gatsby Africa, Bw. Justin Highstead, Januari 22, 2026, jijini Dodoma. 

Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati, kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa kiufundi utakaochechemua ufanisi katika sekta ya mipango na uwekezaji nchini. 

Dkt. Chaya ameipongeza Gatsby Africa kwa kuwa mshirika imara katika utekelezaji wa programu mbalimbali za maendeleo zinazoongozwa na Ofisi ya Rais, mipango na uwekezaji.

Kwa upande wake Bw. Highstead amesisitiza utayari wa Gatsby kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali, akisifu mazingira wezeshi na utayari wa OR-MU katika kurahisisha utekelezaji wa miradi ya pamoja.

 





Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA