MBUSULE BOY: MUZIKI NI MAISHA NA BIASHARA – AJA NA “MAJI YA MOTO”

 


Msanii chipukizi anayekuja kwa kasi kwenye muziki wa Bongo, Mbusule Boy, jina lake halisi Kelvin Juma, ametambulisha rasmi wimbo wake mpya unaoitwa “Maji ya Moto.” 

Ametokea Mwanza na kwa sasa anaishi Dar es Salaam ambako anaendelea kukuza kipaji chake cha muziki kwa bidii.

Mbusule Boy yupo chini ya lebo ya Bank Boys Record inayomilikiwa na Don Cash, ambaye pia ni meneja wake. 

Kupitia usimamizi huo, tayari ameachia jumla ya nyimbo sita zinazopatikana kwenye majukwaa yote ya kidijitali.

Mbali na “Maji ya Moto,” nyimbo zake nyingine ni pamoja na Uzuri Wako, Katoto, Nasikia Raha, Unaniumiza na Mimi na Wewe. 

Wimbo wa “Maji ya Moto” umetolewa Februari 2026, ukiwa umetayarishwa na Mbusuleba huku mtunzi na mtayarishaji wa mashairi akiwa ni Kelvin Juma mwenyewe.

Msanii huyo amesema muziki kwake ni maisha na pia ni biashara, na amewaomba Watanzania kumpokea na kumshika mkono katika kila hatua ya safari yake ya muziki, akiahidi kuendelea kutoa kazi bora zenye ubunifu na mvuto wa kipekee.
Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA