Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini Seleman Bungara (Bwege) amefariki Dunia mchana huu, akiwa kwenye Hospitali moja ya binafsi huko Kigamboni, Dar es Salaam
Kaka wa marehem Abbas S.A. Bungara amesema marehemu alifikishwa Hospitalini hapo kwaajili ya kufanyika Dialysis kama ilivyokuwa ikifanyika kawaida, na ndipo umauti ulivyomfika,
Aidha kwa sasa mipango ya mazishi inaendelea, na taarifa zaidi zitatolewa hapo baadae ila msiba (kwaajili ya watu kuhani) ni Temeke nyumbani kwa Abbas Bungara,
Enzi za uhai wake marehemu Bwege amewahi kutumikia vyama vya siasa vya CUF, ACT Wazalendo na hivi karibuni alitangaza kujiunga na CHADEMA, ingawa mchakato rasmi wa kukabidhiwa kadi ya chama hicho ulikuwa haujakamilika.

إرسال تعليق