NAIBU WAZIRI MAKONDA AWATAKA MAAFISA HABARI KUHABARISHA UMMA SHUGHULI ZA SERIKALI

 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amewasisitiza maofisa habari nchini kuimarisha uwajibikaji wao kwa kutoa taarifa za mara kwa mara kwa wananchi kuhusu shughuli zote zinazotekelezwa na Serikali, katika maeneo yao.

Makonda ametoa kauli hiyo leo Desemba 15, 2025, jijini Dodoma, alipokutana na Menejimenti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika Ofisi za Wizara zilizopo Mji wa Serikali Mtumba.

Amesema Wizara ya Habari ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi katika kutangaza, kufafanua na kusemea utekelezaji wa ahadi na mipango ya maendeleo, hivyo maofisa wake wanapaswa kutimiza wajibu wao kwa weledi, uwazi na kwa kuzingatia masilahi ya umma.

“Wananchi wana haki ya kujua kinachofanyika na Serikali yao. Maofisa Habari mna wajibu wa kuhakikisha taarifa sahihi, kwa wakati na zilizo wazi zinawafikia wananchi ili kuimarisha uelewa na imani kwa Serikali,” amesema.

Kwa upande wake, Menejimenti ya Wizara imeahidi kuendelea kushirikiana na maofisa habari katika ngazi zote ili kuboresha mifumo ya mawasiliano ya Serikali, ikiwamo matumizi ya majukwaa ya kidijitali, ili wananchi wapate taarifa kwa haraka na kwa ufanisi.

Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 تعليقات

إرسال تعليق

Post a Comment (0)

أحدث أقدم

TUTUMIE UJUMBE HAPA