CHAMA HAKITASITA KUCHUKUA HATUA PINDI ITAKAPOBAINIKA KUNA UZEMBE - KIHONGOSI

 

 

Na, Mwandishi wetu - Singida

 

 Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amesema Chama hicho hakitasita kuchukua hatua pindi itakapobainika kuna uzembe katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Kihongosi ametoa kauli hiyo leo Januari 20, 2026, wakati akizungumza na Mabalozi wa Shina namba 8 katika eneo la Iguguno, wilayani Mkalama, mkoani Singida, ambapo ameweka wazi kuwa wajibu wa kwanza wa CCM ni kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo yanayogusa maisha yao moja kwa moja.


Amesema ufuatiliaji wa miradi ya serikali ni jukumu la chama, na kwamba kila fedha inayotolewa lazima ionekane kwenye ubora wa mradi husika.


"Tutaangalia ubora na fedha iliyoletwa, na kama kuna uzembe wa aina yoyote tutachukua hatua mara moja, kwa sababu chama hiki wajibu wake ni kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo," amesema Kihongosi.

 

Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA