Picha mbalimbali zikimuonesha Kamishna wa Kamisheni ya Polisi Jamii, Alex Sospeter Mkama, akikabidhiwa rasmi ofisi ya Kamisheni hiyo leo tarehe 30 Machi 2026 katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dodoma.
Hafla hiyo ya makabidhiano imefanywa na aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ulrich Matei, ambaye alimkabidhi majukumu hayo kwa utaratibu rasmi.
Makabidhiano hayo yanaashiria mwanzo wa uongozi mpya wa Kamisheni ya Polisi Jamii chini ya CP Mkama, huku yakilenga kuendeleza na kuimarisha ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na jamii katika kudumisha amani na usalama nchini.
Post a Comment