WANANCHI WAHOJI UHALALI WA VIPIMO VYA BANDO NA DAKIKA ZA MAONGEZI

 



Na Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) kuingilia kati na kusimamia ipasavyo matumizi sahihi ya vipimo vya vifurushi vya intaneti “bando” pamoja na muda wa maongezi wakidai kupoteza data zao kwa haraka na bila uwazi.

Wananchi hao wametoa wito wa kuwepo kwa uwazi na ukomo sahihi wa muda wa matumizi ya data, wakisema ni haki yao kupata kile wanacholipia.

Baadhi ya wakazi waliozungumza jijini hapa wameeleza kusikitishwa na namna megabytes (MBs) au gigabytes (GBs) wanazonunua zinavyoisha kwa muda mfupi hata pale wanapokuwa hawatumii simu zao kikamilifu, jambo linaloashiria kasoro kwenye usahihi wa vipimo hivyo

Meneja wa Wakala wa vipimo mkoa wa Dodoma Said Ibrahim, anasema wakala umepokea maoni hayo ya wadau na kuongeza kuwa umeshaanza mchakato wa kusimamia uhakiki ikiwemo katika vifurushi vya intaneti (Bando) na muda wa maongezi.




Je?, UNA HABARI,PICHA, TANGAZO AU TAARIFA AMBAYO UNGEPENDA TUICHAPISHE KATIKA MTANDAO HUU? WASILIANA NASI, Email : fichuziblog@gmail.com , Simu +255 752 925 603

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post

TUTUMIE UJUMBE HAPA